Jua huipenyeza nuru, <br />Nuru njema ya asubuhi, <br />Hupenya ndani ya moyo wangu, <br />Kuamsha matumaini, <br />Na hisia mpya. <br /> <br />Moyoni yupo mtu mmoja, <br />Wa pekee, <br />Asiye nacho kifani, <br />Kwa maisha yangu yote, <br />Humu duniani. <br /> <br />Kwa sababu, <br />Umeamsha hisia mpya, <br />Hisia ziujazazo moyo wangu, <br />Kunipa mawazo, <br />Huku nikiwa na faraja. <br /> <br />Nimeamini tangu siku ile, <br />Ya kwanza tulipokutana, <br />Kuwa kwa hakika, <br />Utakuwa wangu, <br />Kwa sababu, <br />Unastahili hivyo.<br /><br />Fadhy Mtanga<br /><br />http://www.poemhunter.com/poem/utakuwa-wangu/