Hatimaye mabingwa wa ligi kuu Tanzania Bara Simba SC wamepoteza mchezo wa kwanza wa ligi hiyo msimu huu baada ya kucheza michezo 28 bila kupoteza.<br /><br />Simba wamefungwa bao 1-0 na Kagera Sugar, kwenye mchezo uliopigwa dimba la Taifa Dar es Salaam na kushuhudiwa na Rais Magufuli ambaye alikuwa mgeni rasmi.<br /><br />Bao pekee la Kagera limefungwa dakika ya 85 ya mchezo na Edward Christopher huku Simba wakipoteza mkwaju wa penati uliopanguliwa na kipa wa Kagera, Juma Kaseja.<br /><br />Baada ya mchezo huo Rais Magufuli ameikabidhi Simba kombe la ubingwa wa VPL msimu wa 2017/18 huku akieleza kutoridhishwa na kiwango alichoshuhudia