Kikosi cha Yanga kimeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya African Lyon katika mchezo wa kirafiki uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.<br /><br />Bao pekee la Yanga limewekwa kimiani na Yusuph Mhilu mnamo dakika za mwisho za mchezo.<br /><br />Yanga wametumia mechi hiyo kama maandalizi ya kujiandaa na mechi zijazo za Ligi Kuu Bara.<br /><br />Katika kipute hicho, Yanga imewakosa nyota wake baadhi ikiwemo Kelvin Yondani, Thaban Kamusoko, Juma Mahadhi walio majeruhi na wengine waliokuwa Uganda kwa majukumu ya timu ya taifa.